Mipango mingine ya Bondia Manny Pacquiao ni yeye na Siasa, baada ya Ubunge anaingia na huku..


October 6, 2015
Jana jumatatu bondia maarufu duniani Manny Pacquiao aliweka wazi mikakati yake ya kuingia kwenye siasa baada ya kutangaza kuwania nafasi ya Useneta katika moja ya majimbo nchini kwake Ufilipino.
Staa huyo kwenye Mchezo wa Boxing alitangaza kuwa atagombea nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka 2016 ingawa bado hajaweka wazi atagombea kupitia chama gani.
Bondia huyo maarufu kama Pac Man alikuwa mmoja wa wawakilishi kwenye bunge la nchi hiyo baada ya kuchaguliwa na wananchi wa wilaya yake.
manny-pacquiao-post-fight
Pacquiao na Mayweather.
Pacquiao alifanikiwa kushinda mataji nane ya dunia kupitia mchezo wa ngumi lakini alishindwa katika pambano lake la mwisho dhidi ya mpinzani wake Floyd Mayweather,ikiwa ni moja ya mapambano ya kifahari kufanyika duniani katika jiji la Las Vegas, Marekani.
.

Advertisement

0 comments:

Post a Comment

 
Top